Ee Bwana nitakutukuza,kwa maana umeniinua
Unisafishe kwa hisopo nami nitakuwa safi,unioshe nami nitakuwa mweupe kuliko theluji
Ee Mungu uniumbie Moyo safi,
uifanye upya Roho iliyotulia ndani yangu
usinitenge na uso wako wala Roho yako Mtakatifu usiniondolee
unirudishie furaha ya wokovu wako,
unitegemeze kwa roho ya wepesi
Ee Mungu unichunguze uujue moyo wangu,
unijaribu uyajue mawazo yangu,uone kama iko njia iletayo majuto ndani yangu
ukaniongoze katika njia ya milele
Unifanye kusikia fadhili zako asubuhi,kwa maana nimekutumaini wewe
Unijulishe njia nitakayoiendea,kwa maana nakuinulia nafsi yangu Isa 48:17
Uniponye na adui zangu maana nimekukimbilia wewe
Unifundishe kuyatenda mapenzi yako kwa maana ndiwe Mungu wangu
Roho yako mwema aniongoze kwenye nchi sawa
Mawazo ya moyo wangu na maneno ya kinywa changu
yapate kibali mbele zako Ee Mungu mwokozi wangu
Uniwezeshe kukaa kwako na kukuhimidi daima,
nguvu zangu zote na zitoke kwako
na kila
nitakachokifanya leonikifanye katika nguvu za Roho wako Mtakatifu
Unitumie vile utakavyobaba,
mapenzi yako juu ya maisha yangu kwa siku ya leo yakatimie
Niwezeshe kutumika kwa upole,utii na unyenyekevu nikitembea na wewe daima
sikuzote na siku moja tupate kufurahi pamoja na watakatifu wako mbinguni.AMINA
No comments:
Post a Comment